Mbunge Mathayo Kuongeza michezo mashindano ya jimbo Cup

MBUNGE wa jimbo la Musoma mjini, Vedastus Mathayo (CCM), ameongeza michezo zaidi kwenye mashindano ya Jimbo yatakayofanyika baadae mwaka huu na kuzitaka Kata 16 zinazounda jimbo hilo kuanza kujiandaa kushiriki na kujipatia zawadi mbalimbali.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kata ya Mshikamano, alisema mwaka huu mashindano anayoandaa yataendelea kama kawaida na yataboreshwa zaidi kwa kuongeza michezo mingi tofauti na ilivyokuwa kwenye mchezo wa soka pekee.
Amesema licha ya mchezo wa soka lakini pia kwa mwaka huu kutakuwa na mchezo wa mpira wa pete,riadha,kupiga makasia kwenye mitumbwi,drafti,darts,kukimbia kwenye magunia pamoja na kufukuza kuku na kutoa wito kwa kila mmoja kujiandaa.
Mathayo alisema michezo ni kitu ambacho kwa upande wake anakipenda na kudai mara baada ya kuifanikisha timu ya Biashara United kucheza ligi kuu msimu ujao sasa ni zamu ya wananchi wote wa jimbo la Musoma mjini kupata burudani ya kila mchezo pamoja na zawadi.
Alisema kila Kata itapata jezi pamoja na mipira kwaajili ya kuzitumia kwenye mashindano hayo na maandalizi na mipango ya kufanyika kwa mashindano hayo inakwenda vizuri ili kuyafanya mashindano hayo kuwa na nguvu kubwa.
“ Vijana naomba mjiandae kwaajili ya mashindano ya jimbo na mwaka huu kutakuwa  na michezo mingi na kila mchezo utakuwa na zawadi yake kikubwa muanze maandalizi na naamimi madiwani wa kila Kata wataziandaa timu vizuri.
“ Mwaka huu sio vijana tu hata wazee wetu watashiriki maana kutakuwa na mashindano ya drafti na kukimbia kwenye magunia pamoja na darts naamini huko wazee wetu hawatakosekana nao pia watapata zawasi kupitia mashindano hayo,”alisema Mathayo.
Diwani wa Kata ya Nyasho ambaye pia ni mjumbe wa mkutano mkuu wa TFF, Haji Mtete (CCM), alisema Mathayo amekuwa akichangia kuinua michezo katika mji wa Musoma kupitia mashindano ya jimbo na anastahili kuungwa mkono na wadau wengine.

Nao vijana walioshiriki mkutano huo wamefarijikia na kusikia ujio wa mashindano hayo na kudai watajiandaa mapema ili kuweza kushiriki mashindano hayo na kupata zawadi zitakazotolewa na mbunge huyo kwa washindi.



Mathayo akiwa na wachezaji wa timu ya Biashara walipokuwa kwenye mazoezi kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma

No comments

Kamati zapewa mafunzo ya kupambana na ukatili

KAMATI za kupambana na masuala ya ukatili wa kijinsia katika halmashauri ya wilaya ya Rorya zimepewa mafunzo ya kupambana na masuala ya ...

Powered by Blogger.