Muhongo awaongoza wananchi kuchangia mifuko 500 ya saruji kwa ujenzi wa zahanati

 




MBUNGE wa jimbo la Musoma vijijini, Profesa Sospeter Muhongo, amewaongoza madiwani pamoja na wananchi wa jimbo hilo kuchangia vifaa vya ujenzi ikiwemo mifuko 500 ya saruji,nondo na misumali katika kukamilisha ujenzi wa zahanati na nyumba ya mganga katika vijiji vya Kurwaki na Kigera Etuma.
 
Akizungumza mara baada ya kuendesha zoezi hilo katika ziara yake ya siku 3 jimboni, alisema suala la afya za wananchi ni suala muhimu ambalo ni moja ya vipaumbele vyake katika kuhakikisha wananchi wanakuwa na afya njema ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.
Amesema adhima ya serikali ni kuhakikisha kila Kijiji kinakuwa na zahanati kwaajili ya kuwapa huduma wananchi nay eye kama mbunge anayewajali wananchi wake atahakikisha anatoa ushirikiano unaohitajika katika kufanikisha na kupatikana huduma za afya kwenye kila eneo.
 
Muhongo ambaye alichangia zaidi ya mifuko 300 kwenye zahanati ya vijiji hivyo pamoja na vifaa vingine vya ujenzi,alisema wananchi pia wanapaswa kuchangia na sio kuisubilia serikali kuwafanyia kila jambo huku wenyewe wakikaa pembeni.
Alisema bila kuwa na afya njema mwananchi hawezi kushiriki shughuli za maendeleo hivyo kuendelea kuwa masikini suala ambalo anapambana nalo kuhakikisha wananchi wanakuwa na uchumi mzuri na kusomesha watoto.
“ Pamoja na kipaumbele kikubwa cha elimu katika jimbo letu lakini afya ni suala la msingi ambalo tunapaswa kulizingatia kuhakikisha wananchi wanakuwa na afya njema na wanapata huduma za afya katika maeneo yao ya karibu katika kuunga mkono juhudi za serikali.
“ Niwashukuru madiwani na wananchi katika kuunga mkono juhudi hizi kwa kuchangia kadri mnavyoweza ili vijiji vyetu viweze kupata zahanati na nyumba za waganga wanaotuhudumia maana bila kuwa na afya njema hatuwezi kushiriki shughuli za maendeleo,”amesema Muhongo.
 
 

Mwenyekiti wa halmashauri ya Musoma, Charles Magoma, amesema Muhongo amekuwa akifanya juhudi kubwa katika shughuli za maendeleo na katika zahati tayari ameshachangia katika ujenzi wa zahanati 9 ambazo zinaendelea kujengwa ambazo zitasaidia kusogeza huduma kwa wananchi na kuahidi kuendelea kumuunga mkono.
 
Diwani wa Kata ya Nyakatende, Rufumbo Mgini, amesema Kata yake ambayo ina vijiji 4 ilikuwa haina zahanati hata moja tangu kupata uhuru rakini jitihada za mbunge Muhongo zimefanikisha kupatikana kwa zahanati katika Kijiji cha Kigera Etuma pamoja na nyumba ya Mganga hivyo kuwapunguzia adha wananchi ya kutembea umbali waa kilometa


 Akimalizia ziara yake kwenye Kata ya Nyegina, Muhongo aliwashukuru wananchi wa zawa wa Musoma vijijini kwenye maeneo ya Nyegina na Mkirira kwa kushirikiana kuchangia jumla ya shilingi milioni 1.6 na mifuko 238 ya saruji kwaajili ya zahanati ya Kijiji cha Mkirira ambapo jimbo limebuni mbinu mpya ya kushirikiana na serikali kuleta maendeleo makubwa ya kiuchumi na kijamii kwa kuwashirikisha wananchi walipo ndani na nje ya jimbo hilo.


No comments

Kamati zapewa mafunzo ya kupambana na ukatili

KAMATI za kupambana na masuala ya ukatili wa kijinsia katika halmashauri ya wilaya ya Rorya zimepewa mafunzo ya kupambana na masuala ya ...

Powered by Blogger.