Benki ya NMB yawaita wakulima wa pamba kufungua akaunt


 



BENKI ya NMB wilayani Bunda imewaita wakulima wa zao la pamba kufungua akaunti kwenye benki hiyo ili kuweza kupitiishiwa malipo yao ya ununuzi wa zao hilo katika msimu wa ununuzi utakaonza mei mosi mwaka huu.
 
Akizungumza kwenye mkutano wa utoaji elimu kwa wakulima kabla ya kuanza kwa msimu wa ununuzi uliongozwa na mkuu wa wilaya ya Bunda, Lyidia Bupilipili, kwenye vijiji vya Hunyari, Kiroleli na Nyamswa,meneja wa NMB tawi la Bunda,Antipas Nnko, amesema wakulima wasiwe na wasiwasi na benki hiyo kwa kuwa fedha zao zitakuwa sehemu salama.
 
Amesema inayo fursa ya akaunti ya chapchap ambayo inafunguliwa bure na watawafata wakulima kwenye maeneo yao na kinachohitajika ni kuwa na kitambulisho cha taifa au barua ya utambulisho kutoka kwa mtendaji wa Kata.

Nnko amesema wanunuzi wote wa pamba wanazo akaunt kwenye benki hiyo hivyo itakuwa rahisi kuhamisha fedha kutoka akaunt moja kwenda akaunti nyingine kuliko kufungua akaunt kwenye benki nyingine.

MKUU wa wilaya ya Bunda, Lyidia Bupilipili, akisisitiza umuhimu wa kufungua akaunt kwa kuwa malipo yote ya ununuzi wa pamba msimu huu yatapitia benki



 

Kaimu meneja wa Wakala wa Vipimo mkoa wa Mara, Jacob Lyambo, akitoa elimu ya mizani kwenye mkutano na wakulima wa pamba wilayani Bunda

 Wakulima wa pamba wakifatilia elimu enayotolewa


No comments

Kamati zapewa mafunzo ya kupambana na ukatili

KAMATI za kupambana na masuala ya ukatili wa kijinsia katika halmashauri ya wilaya ya Rorya zimepewa mafunzo ya kupambana na masuala ya ...

Powered by Blogger.